Mtume Muhammad (s.a.w) amesema: "Ubora wa Qur'an juu ya maneno mengine,ni kama vile ubora wa Mwenyezi Mungu juu ya viumbe wake" Jaamiul-Akhbaar.
Na amesema pia:" Pindi mwalimu anaposema kumwambia mtoto(mwanafunzi), BISMILLAH -RAHMAN RAHIYM, na mtoto akasema; BISMILLAH-RAHMAN RAHIYM, Mwenyezi Mungu humuandikia mtoto huyo na wazazi wake na mwalimu wake kuwa huru na moto wa Jahannam" Majmaul-Bayaan Juzuu ya 1 Sahifa ya 18.
Imam Jaafar Sadiq (a.s) amesema: " Kusoma Qur'an katika Msahafu huwapunguzia wazazi wawili adhabu(za kaburini), hata kama wao ni makafiri" Al-Kaaf Juzuu ya 1 Sahifa ya 440.
Na Imam Ali bin Abi Talib(a.s) amesema: "Mwenye kusoma Qur'an katika umma huu kisha akaingia motoni, basi (mtu) huyo ni miongoni mwa wale ambao huzichukulia aya za Mwenyezi Mungu kuwa ni upuuzi" Tafsirul-Iyaash.
Hivyo basi, inampasa kila muislam kuitukuza Qur'an Tukufu,na kuisoma na kuwafundisha watoto wetu ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu duniani na akhera.
NURU YENYE HEKIMA ni blog inayoelezea habari,matukio na mafundisho juu ya dini ya Kiislam ili kuwahabarisha na kuwaelimisha waislamu kuhusu dini yao, na kuwafanya waweze kuishi katika dunia hii kwa salama na amani kabla ya kwenda kwenye maisha ya milele ambayo ni maisha ya Akhera.
Jumapili, 22 Septemba 2013
Ijumaa, 20 Septemba 2013
ULAZIMA WA KUFANYA KAZI KATIKA UISLAM
Uislam ni mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu ambao umejikita katika nyanja mbalimbali za maisha,kama vile; uchumi, siasa, utamaduni na ustawi wa jamii. Katika suala zima la kiuchumi, uislam unamtaka muislam kufanya kazi ya halali, ili kujipatia kipato kitakachomwezesha yeye kukidhi mahitaji yake muhimu ya maisha.
Amepokea Ibnu Jarir kutoka kwa Ammarah bin Khuzaimah bin Thabit, amesema: Nilimsikia Umar bin Khattab anamwambia baba yangu: "Nini kinakuzuia kupanda ardhi yako?" Baba yangu akasema: "Mimi ni mzee nitakufa kesho" Umar akamwambia: "Nakuhimiza uipande" Hakika mimi nilimuona Umar na baba yangu wakiipanda.
Na kutoka kwa Imam as-Sadiq (a.s) amesema: " Hakika mimi najituma katika haja ambayo amenitosheleza kwayo Mwenyezi Mungu, siifanyi isipokuwa ni kwasababu yakutaka Mwenyezi Mungu anione najitolea katika kutafuta halali, je husikii kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Inapomalizika swala tawanyikeni katika ardhi na tafuteni fadhila za Mwenyezi Mungu..."
Hivyo ni muhimu kwa kila muislam kuhakikisha kuwa anajituma kwa bidii, katika kufanya kazi ya halali mfano; kilimo, uvuvi, biashara n.k ili kupata mahitaji muhimu ya maisha yake na kuepuka kuleta visingizio visivyokuwa na maana.
Amepokea Ibnu Jarir kutoka kwa Ammarah bin Khuzaimah bin Thabit, amesema: Nilimsikia Umar bin Khattab anamwambia baba yangu: "Nini kinakuzuia kupanda ardhi yako?" Baba yangu akasema: "Mimi ni mzee nitakufa kesho" Umar akamwambia: "Nakuhimiza uipande" Hakika mimi nilimuona Umar na baba yangu wakiipanda.
Na kutoka kwa Imam as-Sadiq (a.s) amesema: " Hakika mimi najituma katika haja ambayo amenitosheleza kwayo Mwenyezi Mungu, siifanyi isipokuwa ni kwasababu yakutaka Mwenyezi Mungu anione najitolea katika kutafuta halali, je husikii kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Inapomalizika swala tawanyikeni katika ardhi na tafuteni fadhila za Mwenyezi Mungu..."
Hivyo ni muhimu kwa kila muislam kuhakikisha kuwa anajituma kwa bidii, katika kufanya kazi ya halali mfano; kilimo, uvuvi, biashara n.k ili kupata mahitaji muhimu ya maisha yake na kuepuka kuleta visingizio visivyokuwa na maana.
Alhamisi, 19 Septemba 2013
Dini ya Kiislam inawahimiza waislam kujenga tabia ya kupenda kusoma Qur’an majumbani mwao, ili waweze kupata Baraka mbalimbali zitokanazo na usomaji wa Qur’an, na kuepuka hasara zitokanazo na kutosoma Qur’an majumbani .
Imam Ali bin Abi Talib (a.s) amesema: “Nyumba ambayo husomwa ndani yake Qur’an, na hutajwa humo Mwenyezi Mungu Mtukufu, huongezeka Baraka zake na hutembelewa na Malaika watukufu wa Mwenyezi Mungu, na mashetani huihama;na nyumba hiyo huwapa mwangaza viumbe waliopo mbinguni kama vile nyota zinavyowapa mwangaza waliopo ardhini.
Na hakika nyumba ambayo haisomwi humo Qur’an, wala hatajwi humo Mwenyezi Mungu Mtukufu hupungua Baraka zake,huhama humo Malaika watukufu wa Mwenyezi Mungu na mashetani hufanya makazi katika nyumba hiyo” Al-Kaaf Juzuu ya 2 Sahifa ya 446.
Jumanne, 17 Septemba 2013
FADHILA ZA KUSOMA QUR'AN
fadhila za kusoma qur'anKusoma Qur'an kuna fadhila nyingi sana kwa muislam. Hivyo Mtume(S.A.W) amewahimiza waislam kusoma kila mara, ili wapate manufaa yatokanayo na usomaji huo wa Kitabu hicho Kitakatifu cha Allah Mtukufu.
Miongoni mwa fadhila za kusoma Qur'an ni hizi zifuatazo:
Mtume(S.A.W) amesema,kumwambia Salmaan al-Farsi: " Ewe Salmaan!Jilazimishe sana kusoma Qur'an,kwani kusoma Qur'an ni Kafara kwa ajili ya madhambi na kinga dhidi ya moto na humsahalishia mtu na adhabu za Allah. Na huandikiwa thawabu za mashahidi mia moja,kila mwenye kusoma aya moja na hupewa katika kila Surah anayoisoma thawabu za Manabii na Mitume na Malaika humteremshia rehema kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kumuombea msamaha. Hakika Muumini anaposoma Qur'an, Mwenyezi Mungu Mtukufu humtazama kwa jicho la rehema na humpa kwa kila herufi aisomayo nuru katika Sirat.
"Ewe Salmaan! Pindi Muumin anaposoma Qur'an Mwenyezi Mungu humfungulia milango ya rehema na huumba katika kila herufi inayotoka kinywani mwake Malaika anayemsabihi Mwenyezi Mungu mpaka siku ya Kiyama."
Miongoni mwa fadhila za kusoma Qur'an ni hizi zifuatazo:
Mtume(S.A.W) amesema,kumwambia Salmaan al-Farsi: " Ewe Salmaan!Jilazimishe sana kusoma Qur'an,kwani kusoma Qur'an ni Kafara kwa ajili ya madhambi na kinga dhidi ya moto na humsahalishia mtu na adhabu za Allah. Na huandikiwa thawabu za mashahidi mia moja,kila mwenye kusoma aya moja na hupewa katika kila Surah anayoisoma thawabu za Manabii na Mitume na Malaika humteremshia rehema kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kumuombea msamaha. Hakika Muumini anaposoma Qur'an, Mwenyezi Mungu Mtukufu humtazama kwa jicho la rehema na humpa kwa kila herufi aisomayo nuru katika Sirat.
"Ewe Salmaan! Pindi Muumin anaposoma Qur'an Mwenyezi Mungu humfungulia milango ya rehema na huumba katika kila herufi inayotoka kinywani mwake Malaika anayemsabihi Mwenyezi Mungu mpaka siku ya Kiyama."
HAKI YA MWANAMKE KUMILIKI MALI
Uislam umempa mwanamke haki ya kumiliki mali akiwa kwa mumewe au nyumbani kwao.Ni hivi karibuni jumuia mbalimbali za kiraia zimeanza kumtetea mwanamke ili apewe haki hiyo.
Qur'an Tukufu imeeleza kinagaubaga kuhusu haki hiyo.Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: "Wala msitamani vile ambavyo Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu(kwa vitu hivyo) kuliko wengine.Wanaume wanayo sehemu(kamili) ya vile walivyovichuma; na wanawake nao wanayo sehemu(kamili) ya vile walivyovichuma.Na mwombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu" Surat Nisaa aya ya 32.
Aya hii inaeleza wazi kuhusu haki ya mwanamke kujimilikia mwenyewe mali alioichuma maadamu ni kwa njia ya halali au pengine alipewa zawadi na ndugu zake.haki ya mwanamke kumiliki mali
Na: Abudhar Salim
Qur'an Tukufu imeeleza kinagaubaga kuhusu haki hiyo.Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: "Wala msitamani vile ambavyo Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu(kwa vitu hivyo) kuliko wengine.Wanaume wanayo sehemu(kamili) ya vile walivyovichuma; na wanawake nao wanayo sehemu(kamili) ya vile walivyovichuma.Na mwombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu" Surat Nisaa aya ya 32.
Aya hii inaeleza wazi kuhusu haki ya mwanamke kujimilikia mwenyewe mali alioichuma maadamu ni kwa njia ya halali au pengine alipewa zawadi na ndugu zake.haki ya mwanamke kumiliki mali
Na: Abudhar Salim
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)